Swali: Mimi huenda kuswalia jenaza kila siku na kulisindikiza mpaka makaburini kulizika. Kuna mtu anayenikataza na kusema hili halikufanywa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ni kupetuka mipaka. Je, kunikataza kwake ni sahihi au kitendo changu mimi ndio sahihi?

Jibu: Kukukataza kwake sio sahihi. Kwa kuwa wewe unataka ujira na thawabu juu ya hilo. Unafanya vizuri. Hakuna neno. Kwa tendo lako hili unatarajiwa juu yako kupata thawabu – Allaah akitaka.

Lakini usijipe uzito. Ikiwa kuna uzito juu ya nafsi yako, usijitie uzito.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (10) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1430-10-29.mp3
  • Imechapishwa: 11/11/2014