Wako watu wenye kujishughulisha kukataza ribaa, uzinzi na uharibikaji wa tabia. Ni kweli kwamba mambo haya ni haramu na ni maharibifu. Lakini shirki ni kubwa zaidi. Ni kwa nini hawatilii mkazo kukataza shirki, kutahadharisha kutokamana na shirki na kubainisha yale wanayotumbukia watu ndani yake katika shirki kubwa ilihali huku wanadai kuwa ni waislamu? Ni kwa nini wanachukulia wepesi suala hili la shirki na kupumbaa kwalo na kuwaacha watu wakatumbukia ndani yake ilihali wanachuoni wapo bali wanaishi pamoja na watu hawa na wakawanyamazia? Kwa hiyo ni lazima kujishughulisha kwanza na kukataza khatari hii kubwa iliyouangamiza Ummah vibaya sana. Kila dhambi iliochini yake ni ndogo kuliko hiyo. Lililo la wajibu ni kuanza na la muhimu zaidi kisha kuyaendea ya muhimu mengine baada ya hilo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Thalaath-il-Usuwl, uk. 87
  • Imechapishwa: 08/02/2020