Swali: Ni ipi hukumu ya kuwavisha hirizi watoto au mgonjwa?

Jibu: Haijuzu kufanya hivo. Haijuzu kutundika hirizi. Mgonjwa anatakiwa kusomewa, maji yasomewe na amwagiwe, iandikwe Qur-aan na kutumbukizwa kwenye maji ambayo atayanywa. Hakuna neno. Yote haya ni kujitibu kwa Qur-aan.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (64) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/28-07-1438h-fathou.mp3
  • Imechapishwa: 29/07/2017