Kuwalingania makafiri na wanawake wenye kuvaa vibaya

Swali: Inajuzu kuwalingania wanawake wa kikafiri katika Uislamu hata kama watakuwa wamevaa vibaya? Wengi katika wao wamesilimu.

Jibu: Hili linatokamana na hali ya yule mlinganizi. Ikiwa anachelea juu ya nafsi yake mtihani, hakuna kitu kinacholingana na moyo salama. Na ikiwa yuko na ghera juu ya Uislamu na waislamu, basi anatakiwa kutambua kuwa imani inazidi na kushuka. Wakati fulani mtu anahisi hamasa yenye nguvu juu ya dini, kiasi cha kwamba haathiriwi na kitu. Katika hali hii ni jambo zuri. Ikiwa anachelea juu ya nafsi yake mtihani, basi amuombe mwengine afanye hivo ambaye hachelei juu ya nafsi yake. Allaah akujazeni kheri kwa yale mnayofanya.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://muqbel.net/sounds.php?sound_id=38
  • Imechapishwa: 19/02/2017