Swali: Jambo la kuwafutarisha wafungaji ndani ya Ramadhaan hufanyika kwa wingi na khaswa wafanya kazi. Lakini baadhi yao hawaswali au hawahudhurii swalah ya mkusanyiko msikitini licha ya ukaribu wake. Je, ni sahihi kuwafuturisha mfano wa wafanya kazi hawa ambao ni wahitaji wa futari?

Jibu: Kinachozingatiwa ni kuwafuturisha wale wengi wa wafungaji. Ikiwa wengi wao wanahifadhi swalah basi hawatozingatiwa wale walio pamoja nao ambao pengine hawako hivo. Isitoshe huenda kufanya hivo kukawalingania kutubu.

´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh

´Abdullaah bin Ghudayyaan

Swaalih al-Fawzaan

Ahmad al-Mubaarakiy

´Abdullaah ar-Rukbaan

´Abdullaah al-Mutlaq

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (01/616) nr. (22170)
  • Imechapishwa: 22/04/2022