Swali: Mwenye kuacha mambo ya kisasa; kama kupanda gari na kuishi kwenye manyumba ya kisasa anahesabika kuwa ni katika watu wenye kuipa nyongo dunia?

Jibu: Hapana. Huku ni kujikalifisha na kupetuka mipaka.

قُلْ مَنْ حَرَّمَ زِينَةَ اللَّـهِ الَّتِي أَخْرَجَ لِعِبَادِهِ وَالطَّيِّبَاتِ مِنَ الرِّزْقِ

“Sema: “Nani aliyeharamisha mapambo ya Allaah ambayo Amewatolea waja Wake na, vizuri katika riziki?” (07:32)

Hakuna yeyote anayeharamisha Aliyohalalisha Allaah (´Azza wa Jalla) na kusema kuwa ni kuipa nyongo dunia. Lakini hata hivyo asifanye israfu. Awe kati na kati.

وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا

“Na wale ambao wanapotoa huwa hawafanyi israfu na wala hawafanyi uchoyo na wanakuwa wastani baina ya hayo.” (25:67)

Asifanye israfu na wala asifanye ubakhili. Awe kati na kati. Haya ndiyo Aliyoweka Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) katika Shari´ah. Haijuzu kuharamisha vitu vizuri Alivyoruhusu Allaah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1430-4-23.mp3
  • Imechapishwa: 09/11/2014