Kutoka Malaika wa mauti kwenda virusi vya corona?

Swali: Unasemaje kuhusu kwamba Malaika wa mauti amebadili jina lake kutoka ´Izraa-iyl kwenda Corona?

Jibu: Huku ni kujikakama, maneno ya kipumbavu na yasiyokuwa na maana yoyote. Malaika wa mauti ni Malaika miongoni mwa Malaika wengine na corona ni maradhi miongoni mwa maradhi mengine. Ni vipi mtu anaweza kusema kuwa ni jina la Malaika? Haya ni maneno ya kipumbavu na kujikakama ni jambo ambalo halistahiki kwa mtu kulisema.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=rvZgmJ-Ma4E
  • Imechapishwa: 01/03/2020