Swali: Inajuzu kutoa Zakaat-ul-Fitwr kama vile mchele, mahindi, shayiri na mtama hata kama vitakuwa bado na maganda juu yake?
Jibu: Inajuzu kufanya hivo ikiwa ni miongoni mwa vyakula vinavyoliwa katika mji huo. Hayo ndio maoni sahihi zaidi ya wanachuoni. Lakini inatakiwa iwe baada ya kuvisafisha na maganda. Allaah (Subhaanah) amesema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ
”Enyi walioamini! Toeni katika vizuri mlivyochuma.”[1]
Kwa sababu huku ndio kutakasa dhimma na urafiki zaidi kwa yule fakiri. Isipokuwa tu shayiri si wajibu kuisafisha kutokamana na maganda kutokana na uzito unaopatikana wa kufanya hivo. Lakini pale atapotoa kutoka ardhini shayiri na nafaka nyenginezo mfano wake ambazo manufaa zaidi ni kuziacha kubaki katika maganda yake muda wa kuwa atahakikisha ametekeleza wajibu wake kwa kile kiwango cha uadilifu, basi katika hali hiyo hakuna neno – akitaka Allaah – kwa ajili ya kuchunga manufaa ya bwana na fakiri.
[1] 02:267
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (14/206)
- Imechapishwa: 12/06/2018
Swali: Inajuzu kutoa Zakaat-ul-Fitwr kama vile mchele, mahindi, shayiri na mtama hata kama vitakuwa bado na maganda juu yake?
Jibu: Inajuzu kufanya hivo ikiwa ni miongoni mwa vyakula vinavyoliwa katika mji huo. Hayo ndio maoni sahihi zaidi ya wanachuoni. Lakini inatakiwa iwe baada ya kuvisafisha na maganda. Allaah (Subhaanah) amesema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ
”Enyi walioamini! Toeni katika vizuri mlivyochuma.”[1]
Kwa sababu huku ndio kutakasa dhimma na urafiki zaidi kwa yule fakiri. Isipokuwa tu shayiri si wajibu kuisafisha kutokamana na maganda kutokana na uzito unaopatikana wa kufanya hivo. Lakini pale atapotoa kutoka ardhini shayiri na nafaka nyenginezo mfano wake ambazo manufaa zaidi ni kuziacha kubaki katika maganda yake muda wa kuwa atahakikisha ametekeleza wajibu wake kwa kile kiwango cha uadilifu, basi katika hali hiyo hakuna neno – akitaka Allaah – kwa ajili ya kuchunga manufaa ya bwana na fakiri.
[1] 02:267
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (14/206)
Imechapishwa: 12/06/2018
https://firqatunnajia.com/kutoa-nafaka-kwa-maganda-yake-katika-zakaat-ul-fitwr/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)