Kutoa kafara ya yamini pesa badala ya chakula

Swali: Je, inajuzu kutoa kafara ya yamini mali?

Jibu: Hapana, hili halijuzu. Linaenda kinyume na andiko. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:

فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ

”Basi kafara yake [ya kiapo] ni kulisha maskini kumi… ” (05:89)

Amesema “Lisheni” na hakusema “Toeni swadaqah kwa masikini kumi”. Amesema “Lisheni” ambako maana yake ni kuwapa chakula masikini.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (30) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-6-9.mp3
  • Imechapishwa: 15/11/2014