Swali: Je, nimtahadharisha mlinganizi katika nchi yangu ambaye ana kosa la ´Aqiydah baada ya kuthibiti kosa hili au nisubiri kwanza mpaka waseme wanachuoni wakubwa katika nchi yangu?

Jibu: Ikiwa una uhakika kwamba kweli ana kosa, basi wewe unatakiwa kuwabainishia kwanza huenda akajirudi. Ikiwa ataendelea kung´ang´ania na asijirudi, basi wabainishie watu yale makosa alionayo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (79) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-9-2-1439-01.mp3
  • Imechapishwa: 09/03/2018