Swali: Ambaye amepitwa na Swalah ya al-Fajr pasina khiyari yake na ni katika watu wenye kuhifadhi Swalah ya Jamaa´ah na hakuamka isipokuwa wakati kunapokimiwa kwa ajili ya Swalah ya Ijumaa, kisha akaswali Ijumaa kwa nia ya al-Fajr na baada ya hapo akalipa Dhuhr Rakaa nne. Je, kitendo chake hichi ni sahihi?
Jibu: Hapana, sio sahihi. Alitakiwa kuswali al-Fajr kwanza Rakaa mbili kisha ndio akaswali Ijumaa. Angeanza kuswali al-Fajr kisha ndio akaswali Ijumaa hata kama Ijumaa atawahi Rakaa ile ya mwisho tu. Anatakiwa kuswali al-Fajr kwanza Rakaa mbili kisha aingie pamoja na imamu kwa zile Rakaa zitazokuwa zimebaki za Ijumaa. Ikiwa amewahi Rakaa moja kikamilifu, aitimize kwa sura ya Ijumaa. Ikiwa hakuiwahi [Rakaa moja] kikamilifu, aitimize kwa sura ya Dhuhr.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (06) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_06.mp3
- Imechapishwa: 29/06/2018
Swali: Ambaye amepitwa na Swalah ya al-Fajr pasina khiyari yake na ni katika watu wenye kuhifadhi Swalah ya Jamaa´ah na hakuamka isipokuwa wakati kunapokimiwa kwa ajili ya Swalah ya Ijumaa, kisha akaswali Ijumaa kwa nia ya al-Fajr na baada ya hapo akalipa Dhuhr Rakaa nne. Je, kitendo chake hichi ni sahihi?
Jibu: Hapana, sio sahihi. Alitakiwa kuswali al-Fajr kwanza Rakaa mbili kisha ndio akaswali Ijumaa. Angeanza kuswali al-Fajr kisha ndio akaswali Ijumaa hata kama Ijumaa atawahi Rakaa ile ya mwisho tu. Anatakiwa kuswali al-Fajr kwanza Rakaa mbili kisha aingie pamoja na imamu kwa zile Rakaa zitazokuwa zimebaki za Ijumaa. Ikiwa amewahi Rakaa moja kikamilifu, aitimize kwa sura ya Ijumaa. Ikiwa hakuiwahi [Rakaa moja] kikamilifu, aitimize kwa sura ya Dhuhr.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (06) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_06.mp3
Imechapishwa: 29/06/2018
https://firqatunnajia.com/kuswali-swalah-ya-ijumaa-kwa-nia-ya-fajr/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)