Swali: Kundi la watu waliingia msikitini kabla ya kukimiwa swalah ambapo wakaswali kabla ya Iqaamah. Ni ipi hukumu ya swalah yao?
Jibu: Haijuzu kwa mtu kuanzisha mkusanyiko kwenye msikiti ulio na imamu aliyepangwa isipokuwa kwa idhini ya imamu. Watu hawa wakisema kuwa ni wasafiri na kwamba hawawezi kusubiri mpaka atapokuja imamu na akawaswalisha. Basi tunawaambia kwamba mambo ni sahali; mkiwa ni wasafiri basi endeleeni na safari na swalini njiani. Ama kuswali ndani ya msikiti ulio na imamu rasmi kabla ya kufika imamu ni jambo lisilofaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kufanya hivo na akasema:
“Asimwongoze mtu mwingine katika utawala wake.”
Mtawala wa msikiti ni yule imamu wake. Kwa hivyo ni wajibu kusubiri mpaka pindi imamu atapofika. Wakisema kuwa ni wasafiri na hawawezi kusubiri, basi tunawaambia kwamba ni wenye kupewa udhuru kuacha kuswali swalah ya mkusanyiko na hivyo safirini na swalini mahali kokote mtakotaka.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1327
- Imechapishwa: 07/11/2019
Swali: Kundi la watu waliingia msikitini kabla ya kukimiwa swalah ambapo wakaswali kabla ya Iqaamah. Ni ipi hukumu ya swalah yao?
Jibu: Haijuzu kwa mtu kuanzisha mkusanyiko kwenye msikiti ulio na imamu aliyepangwa isipokuwa kwa idhini ya imamu. Watu hawa wakisema kuwa ni wasafiri na kwamba hawawezi kusubiri mpaka atapokuja imamu na akawaswalisha. Basi tunawaambia kwamba mambo ni sahali; mkiwa ni wasafiri basi endeleeni na safari na swalini njiani. Ama kuswali ndani ya msikiti ulio na imamu rasmi kabla ya kufika imamu ni jambo lisilofaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kufanya hivo na akasema:
“Asimwongoze mtu mwingine katika utawala wake.”
Mtawala wa msikiti ni yule imamu wake. Kwa hivyo ni wajibu kusubiri mpaka pindi imamu atapofika. Wakisema kuwa ni wasafiri na hawawezi kusubiri, basi tunawaambia kwamba ni wenye kupewa udhuru kuacha kuswali swalah ya mkusanyiko na hivyo safirini na swalini mahali kokote mtakotaka.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1327
Imechapishwa: 07/11/2019
https://firqatunnajia.com/kuswali-msikitini-mkusanyiko-kabla-ya-iqaamah-bila-idhini-ya-imamu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)