Swali: Ni kipi kitabu bora kinachozungumzia fitina iliotokea baina ya ´Aliy na Mu´aawiyah (Radhiya Allaahu ´anhumaa)?

Jibu: Sionelei usome kitabu hicho. Naonelea usalimike na usisome kitu katika mambo haya. Yatakupelekea kuwa na kitu ndani ya moyo wako juu ya Maswahabah, ukamtia makosani mmoja na mwingine katika usawa pasi na dalili. Vilevile inaweza kupelekea ukawa na kinyongo au chuki kwa baadhi yao. Mimi sionelei usome vitabu vya fitina.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (04) http://alfawzan.af.org.sa/node/2047
  • Imechapishwa: 13/11/2016