Swali: Baadhi ya watu wanasoma du´aa kwa sauti ya juu ambapo wanawashawishi walioko pambizoni mwao. Ni ipi hukumu ya kitendo chao hichi?
Jibu: Sunnah ni kusoma du´aa kimyakimya ndani ya swalah na kweginepo. Amesema (Subhaanah):
ادْعُوا رَبَّكُمْ تَضَرُّعًا وَخُفْيَةً
“Muombeni Mola wenu kwa unyenyekevu na kwa siri.”[1]
Jengine ni kwa sababu kufanya hivo ndio ukamilifu zaidi katika kumtakasia nia Allaah na kuukusanya moyo katika du´aa. Isitoshe kufanya hivo kunapelekea kutowashawishi waswaliji na wasomaji walioko kando nawe.
Lakini ikiwa du´aa ni ile ambayo kunaitikiwa “Aamiyn” kama mfano wa du´aa ya Qunuut na du´aa ya kuomba mvua, basi imamu anatakiwa kuisoma kwa sauti ya juu ili wasikilizaji waweze kuitikia “Aamiyn”.
[1] 07:55
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (09/397)
- Imechapishwa: 28/07/2021
Swali: Baadhi ya watu wanasoma du´aa kwa sauti ya juu ambapo wanawashawishi walioko pambizoni mwao. Ni ipi hukumu ya kitendo chao hichi?
Jibu: Sunnah ni kusoma du´aa kimyakimya ndani ya swalah na kweginepo. Amesema (Subhaanah):
ادْعُوا رَبَّكُمْ تَضَرُّعًا وَخُفْيَةً
“Muombeni Mola wenu kwa unyenyekevu na kwa siri.”[1]
Jengine ni kwa sababu kufanya hivo ndio ukamilifu zaidi katika kumtakasia nia Allaah na kuukusanya moyo katika du´aa. Isitoshe kufanya hivo kunapelekea kutowashawishi waswaliji na wasomaji walioko kando nawe.
Lakini ikiwa du´aa ni ile ambayo kunaitikiwa “Aamiyn” kama mfano wa du´aa ya Qunuut na du´aa ya kuomba mvua, basi imamu anatakiwa kuisoma kwa sauti ya juu ili wasikilizaji waweze kuitikia “Aamiyn”.
[1] 07:55
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (09/397)
Imechapishwa: 28/07/2021
https://firqatunnajia.com/kusoma-duaa-kwa-sauti-ya-juu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)