Swali: Baadhi ya watuwazima hawawezi kusimama kwa upesi nyuma ya imamu katika swalah. Hivyo wanaanza kusoma al-Faatihah ilihali hawajasimama na kunyooka vizuri kwa sababu imamu anaweza kusema “Allaahu Akbar” kabla ya wao kukamilisha kusoma al-Faatihah. Je, inafaa kwa mswaliji kusoma al-Faatihah kabla hajasimama na kunyooka sawa?
Jibu: Haijuzu kwa mswaliji muweza kusoma al-Faatihah katika hali ya kuketi kwake chini wala katika hali ya kuinuka kwake. Bali ni lazima kwake kuchelewesha kisomo chake mpaka asimame na kunyooka vizuri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Imraan bin Huswayn:
”Swali kwa kusimama. Usipoweza, kwa kukaa. Usipoweza, lalia bavu.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
an-Nasaa´iy pia ameipokea kwa cheni ya wapokezi Swahiyh na akaongeza:
“Asipoweza, basi kwa kuegemea.”
Kuhusu ambaye hawezi hakuna neno kwake kutokana na Hadiyth iliyotajwa.
[1] al-Bukhaariy (1050).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/229)
- Imechapishwa: 26/10/2021
Swali: Baadhi ya watuwazima hawawezi kusimama kwa upesi nyuma ya imamu katika swalah. Hivyo wanaanza kusoma al-Faatihah ilihali hawajasimama na kunyooka vizuri kwa sababu imamu anaweza kusema “Allaahu Akbar” kabla ya wao kukamilisha kusoma al-Faatihah. Je, inafaa kwa mswaliji kusoma al-Faatihah kabla hajasimama na kunyooka sawa?
Jibu: Haijuzu kwa mswaliji muweza kusoma al-Faatihah katika hali ya kuketi kwake chini wala katika hali ya kuinuka kwake. Bali ni lazima kwake kuchelewesha kisomo chake mpaka asimame na kunyooka vizuri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Imraan bin Huswayn:
”Swali kwa kusimama. Usipoweza, kwa kukaa. Usipoweza, lalia bavu.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
an-Nasaa´iy pia ameipokea kwa cheni ya wapokezi Swahiyh na akaongeza:
“Asipoweza, basi kwa kuegemea.”
Kuhusu ambaye hawezi hakuna neno kwake kutokana na Hadiyth iliyotajwa.
[1] al-Bukhaariy (1050).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/229)
Imechapishwa: 26/10/2021
https://firqatunnajia.com/kusoma-al-faatihah-wakati-mtu-anainuka-kwenda-katika-rakaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)