44 – Abu Muhammad bin Swaa´id na Muhammad bin Sulaymaan an-Nu´maaniy wametuhadithia: Muhammad bin ´Amr bin Hannaan ametuhadithia: Baqiyyah bin al-Waliyd ametuhadithia: ´Ubaydullaah bin ´Umar ametuhadithia, kutoka kwa Sa´iyd bin Abiy Sa´iyd al-Maqbariy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Hurayrah aliyeeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Lau nisingeliona uzito juu ya Ummah wangu basi ningeliwafaradhishia kutumia Siwaak pamoja na wudhuu´ na wacheleweshe swalah ya ´Ishaa mpaka theluthi ya usiku au nusu ya usiku. Hakika Allaah (´Azza wa Jall) hushuka katika mbingu ya dunia na anaita mpaka alfajiri inaingia: “Je, kuna mwenye kuomba nimuitikie? Je, kuna mwenye kuomba msamaha nimsamehe? Je, kuna mwenye kutubia nimsamehe?”

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 125-126
  • Imechapishwa: 28/01/2020