14- Muhammad bin Saa´id alisomewa na mimi huku nasikiliza: Muhammad bin Zanbuur al-Makkiy ametuhadithia: Ismaa´iyl bin Ja´far ametuhadithia: Muhammad bin ´Amr ametuhadithia, kutoka kwa Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah aliyeeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mola wetu anashuka katika mbingu ya dunia wakati kunapobaki nusu ya mwisho ya usiku, au theluthi ya mwisho ya usiku, na anasema mpaka alfajiri inaingia au anaondoka msomaji kutoka katika swalah ya  asubuhi: “Ni nani aniombaye nimuitikie? Ni nani aniulizaye nimpe? Ni nani aniombae maghfirah nimghufurie?”[1]

[1] Ahmad (2/504) na Ibn Khuzaymah (1/302) aliyeisahihisha.

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 103
  • Imechapishwa: 16/01/2018