Kuhusiana na Hadiyth kupitia kwa ´Abdul-Maalik bin Ziyaad kutoka kwa Maalik, ameeleza:

28- Muhammad bin al-Hasan bin Kawthar ametuhadithia: Abu ´Aqiyl Ibraahiym bin ´Aliy ametuhadithia: ´Abdul-Malik bin Ziyaad an-Nusaybiy ametuhadithia: Maalik ametuhadithia, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah aliyeeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kusipobaki katika usiku isipokuwa theluthi basi Allaah (´Azza wa Jall) husema: “Ni nani mwenye kuniomba nimuitikie? Ni nani mwenye kunitaka kitu nimpe? Ni nani aniombae maghfirah nimghufurie?”

al-Agharr hakutajwa katika cheni ya wapokezi wake.

Ma´mar bin Raashid pia ameipokea kutoka kwa az-Zuhriy.

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 112
  • Imechapishwa: 02/01/2020