Kusaidia mwanamke katika safari asiyekuwa na Mahram

Swali: Wakati mwingine nakuwa ndani ya ndege najiwa na mtu ambaye anakuwa na bibi kizee, mama yake, ananambia nimfuatilie mpaka atapofika kwenye uwanja wa ndege mwingine na ndugu yangu atampokea kule. Je, nimuitikie kwa mfano wa mambo kama haya?

Jibu: Hapana. Usisaidiane naye katika madhambi na uadui. Haijuzu kwako kufanya hivi. Ni haramu kwako. Ni lazima awe na Mahram.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (35) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-11-09.mp3
  • Imechapishwa: 15/11/2014