Kusafiri na mke mjamzito kwenda katika mji wa kikafiri

Swali: Mimi ni mfanya biashara ambaye ninaishi Morocco na nataka kusafiri kwenda Ufaransa kwa ajili ya biashara. Mke wangu ni mjamzito na wakati fulani anapoteza fahamu na siwezi kumwacha Morocco peke yake na hana yeyote. Je, inajuzu kwangu kusafiri naye kwenda katika miji ya kikafiri?

Jibu: Hakuna neno. Ikiwa mambo ni kama ulivosema, ya kwamba anahitajia mtu wa kuwa pamoja naye na kumsaidia na kwamba anaweza kupatwa na madhara iwapo atabaki peke yake, safiri naye.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (85) http://alfawzan.af.org.sa/ar/node/17635
  • Imechapishwa: 29/06/2018