Kuoa kunamsaidia mwanafunzi kujifunza elimu

Swali: Kuna wanafunzi ambao wanapuuza kuoa na wanasema kuwa kuoa kunamshughulisha mtu na kusoma na kwamba wanawake wengi hii leo hawamsaidii mwanafunzi juu ya kutafuta elimu na badala yake wanamshughulisha. Wanasema kuwa pamoja na kueneza kwa fitina katika kila sehemu hawawezi kutumbukia katika haramu. Una ushauri gani katika hili?

Jibu: Kuoa hakuzuii na kutafuta elimu. Kinyume chake kunamsaidia mtu kutafuta elimu. Kwa sababu mtu anapata kutulia kwa kuoa na anakuwa na nafasi ya kutafuta elimu. Kwa hivyo kuoa kunamsaidia mtu na kujifunza elimu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ighaathat-il-Lahfaan (74) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-25-01-1439H-01.mp3
  • Imechapishwa: 11/11/2017