Swali: Kuna mtu kafunga. Lakini siku moja hakuamka isipokuwa baada ya jua kuzama. Akanywa maji kidogo ili aweze kupata nguvu za kufunga. Je, swawm yake inafaa?

Jibu: Haijuzu kufunga. Kwa sababu swawm ni lazima mtu ajizuie kula, kunywa, jimaa na vifunguzi vingine vyote kuanzia pale kuingia kwa alfajiri. Kwa hiyo huyu swawm yake si sahihi. Lakini himdi zote ni za Allaah swawm ya sunnah jambo lake ni lepesi. Akiamka baada ya alfajiri kuingia na huku amenuia kufunga ima aendelee na nia yake pasi na kula, kunywa wala kufanya chochote katika vifunguzi au ale na kunywa na wala asilipe kitu. Kwa kuwa ni swawm ya sunnah. Akipenda kuifunga anaifunga na akipenda haifungi.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (41) http://binothaimeen.net/content/1504
  • Imechapishwa: 08/10/2018