Kumtangulia ndugu yako kuchumbia katika muda anasubiri majibu

Swali: Mwanaume akimposa mwanamke na familia yake ikamwambia kuwa wataulizia kuhusu hali yake inafaa kwa yeyote kutangulia na kuposa juu ya posa yake?

Jibu: Hapana, mpaka baada ya kukataliwa. Maadamu tayari ameshajua kuwa amemchumbia asimtangulie mpaka baada ya kujua kuwa amekataliwa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (66) http://alfawzan.af.org.sa/node/16524
  • Imechapishwa: 13/08/2017