Swali: Je, lini bora kwa ambaye yuko karibu na msomaji Qur-aan; je, amsalimie na ampe mkono baada ya kumaliza kwake kuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti au bora ni kutomkata kisomo chake na kumshughulisha na kisomo?
Jibu: Sunnah ni yeye kusalimiwa na kupewa mkono. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Watapokutana waislamu ambapo wakapeana mikono, basi yanapukuchika madhambi yao kama yanavopukuchika kutoka kwenye mti wenye majani makavu.”
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakikutana basi wanapeana mikono na wanapofika kutoka safarini wanakumbatiana.”[1]
Amepokea ad-Daaraqutwniy. Wapokezi wake ni wenye kujengewa hoja katika “as-Swahiyh”.
Jengine ni kwa sababu katika kufanya hivo kuna kuyasisitiza yale mapenzi, kuliwazana na kufahamiana kati ya waislamu. Kukata kisomo kutokana na manufaa yaliyozuka ni jambo linalotakikana.
[1] Haythamiy (08/36) na akasema:
”Ameipokea ad-Daaraqutwniy katika ”al-Awsatw na wapokezi wake ni wapokezi wa Swahiyh, ameipokea pia al-Bayhaqiy (07/100) na katika ”Silsilah Ahaadiyth as-Swahiyhah” (160) ya al-Albaaniy.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/433)
- Imechapishwa: 19/11/2021
Swali: Je, lini bora kwa ambaye yuko karibu na msomaji Qur-aan; je, amsalimie na ampe mkono baada ya kumaliza kwake kuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti au bora ni kutomkata kisomo chake na kumshughulisha na kisomo?
Jibu: Sunnah ni yeye kusalimiwa na kupewa mkono. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Watapokutana waislamu ambapo wakapeana mikono, basi yanapukuchika madhambi yao kama yanavopukuchika kutoka kwenye mti wenye majani makavu.”
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakikutana basi wanapeana mikono na wanapofika kutoka safarini wanakumbatiana.”[1]
Amepokea ad-Daaraqutwniy. Wapokezi wake ni wenye kujengewa hoja katika “as-Swahiyh”.
Jengine ni kwa sababu katika kufanya hivo kuna kuyasisitiza yale mapenzi, kuliwazana na kufahamiana kati ya waislamu. Kukata kisomo kutokana na manufaa yaliyozuka ni jambo linalotakikana.
[1] Haythamiy (08/36) na akasema:
”Ameipokea ad-Daaraqutwniy katika ”al-Awsatw na wapokezi wake ni wapokezi wa Swahiyh, ameipokea pia al-Bayhaqiy (07/100) na katika ”Silsilah Ahaadiyth as-Swahiyhah” (160) ya al-Albaaniy.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/433)
Imechapishwa: 19/11/2021
https://firqatunnajia.com/kumsalimia-ambaye-anasoma-qur-aan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)