Swali: Je, Sunnah ni kuharakisa jeneza au kuchelewesha ili watu wakusanyike?
Jibu: Sunnah ni kuharakisha isipokuwa pakiwa sababu. Wanachuoni wamesema kuwa imependekezwa kuharakisha. Imekuja katika Hadiyth:
“Haitakikani maiti ya muumini kubakizwa juu ya migongo ya famili yake.”
Wanachuoni wamesema kwamba isipokuwa tu akifa ghafla. Basi katika hali hiyo atacheleweshwa mpaka ihakikishwe sababu ya kifo chake, jambo ambalo hufanyika katika mahospitali ya sasa. Kupitia ucheleweshwaji mdogo usiodhuru ambao kwa ajili yake watu wamekusanyika kwa ajili ya kuja kutoa pole itapata kutambulika sababu ya kifo chake. Hapo ni pale ambapo wakati utakuwa sio mrefu. Ama kumchelewesha kwa muda mrefu ni jambo lisilotakiwa.
Haitakikani kuchelewesha jeneza lake. Lakini kwa mfano akicheleweshwa kuanzia alfajiri mpaka adhuhuri, kuanzia adhuhuri mpaka alasiri, ni sawa. Ama kumchelewesha kwa siku moja au mbili ni jambo lisilotakiwa.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
- Imechapishwa: 28/06/2019
Swali: Je, Sunnah ni kuharakisa jeneza au kuchelewesha ili watu wakusanyike?
Jibu: Sunnah ni kuharakisha isipokuwa pakiwa sababu. Wanachuoni wamesema kuwa imependekezwa kuharakisha. Imekuja katika Hadiyth:
“Haitakikani maiti ya muumini kubakizwa juu ya migongo ya famili yake.”
Wanachuoni wamesema kwamba isipokuwa tu akifa ghafla. Basi katika hali hiyo atacheleweshwa mpaka ihakikishwe sababu ya kifo chake, jambo ambalo hufanyika katika mahospitali ya sasa. Kupitia ucheleweshwaji mdogo usiodhuru ambao kwa ajili yake watu wamekusanyika kwa ajili ya kuja kutoa pole itapata kutambulika sababu ya kifo chake. Hapo ni pale ambapo wakati utakuwa sio mrefu. Ama kumchelewesha kwa muda mrefu ni jambo lisilotakiwa.
Haitakikani kuchelewesha jeneza lake. Lakini kwa mfano akicheleweshwa kuanzia alfajiri mpaka adhuhuri, kuanzia adhuhuri mpaka alasiri, ni sawa. Ama kumchelewesha kwa siku moja au mbili ni jambo lisilotakiwa.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
Imechapishwa: 28/06/2019
https://firqatunnajia.com/kumchelewesha-maiti-kidogo-kwa-sababu-ya-uchunguzi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)