Swali: Ni ipi hukumu kwa yule mwenye kumbusu mke wake akiwa na twahara na anataka kuswali?

Jibu: Hakuna kitu juu yake. Akimbusu mke wake na asitokwe na kitu wudhuu´ wake ni sahihi kutokana na maoni yenye nguvu. Baadhi ya wanachuoni wameona kuwa kumbusu kunachengua wudhuu´. Wengine wakasema kuwa kule kumgusa tu kunachengua wudhuu´. Maoni ya sawa ni kwamba hakuchengui wudhuu´ kutokana na maoni yenye nguvu zaidi ya wanachuoni: kwamba kumgusa mwanamke au kumbusu hakuchengui wudhuu´ midhali hakutokwa na kitu si madhiy wala kingine.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa ad-Duruus https://binbaz.org.sa/fatwas/3788/%D9%87%D9%84-%D8%AA%D9%82%D8%A8%D9%8A%D9%84-%D8%A7%D9%84%D8%B2%D9%88%D8%AC%D8%A9-%D9%8A%D9%86%D9%82%D8%B6-%D8%A7%D9%84%D9%88%D8%B6%D9%88%D8%A1
  • Imechapishwa: 21/03/2020