Swali: Je, inajuzu kula kabla ya adhaana katika Ramadhaan kwa dakika tano au kumi?

Jibu: Ikiwa adhaana inaenda sambamba na wakati, haijuzu kula kabla yake. Ama ikiwa adhaana inakawia wakati wake, kwa mwenye yakini na ni kuwa anaona kuzama kwa jua ataegemea kunako asili. Kwa kuwa kufuturu baada tu ya kuzama kwa jua moja kwa moja kufanya hivi ndio bora.

“Watu wataendelea kuwa juu ya kheri muda wa kuwa wanafanya haraka  kukata swawm.”

Watu wa nyumba na familia hii wanakuwa katika kheri kubwa. Allaah awajaalie kheri na baraka. Jitofautisheni na Rawaafidhw Shiy´ah na shikamaneni bara bara na Sunnah na harakisheni kufuturu.

  • Mhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://alwasabi.al3ilm.com/alfatawaa
  • Imechapishwa: 10/05/2020