Swali: Nyumbani kwetu kuna dishi, video na mfanyakazi wa kike. Baba yangu na ndugu zangu wengine hawaswali si nyumbani wala msikitini. Vilevile wanavuta sigara. Nimewanasihi mara nyingi kwa yote haya lakini hata hivyo haikufua dafu. Mimi ninapowaendea basi ninanyongeka sana kwa sababu mfanyakazi huyu  wa kike anafunua uso wake, anaacha kichwa wazi na dishi inakuwepo na sauti imepandishwa juu ya kwa muziki. Nifanye nini? Naomba uwaombee du´aa waongoke.

Jibu: Ninawaombea kwa Allaah awaongoze na ndugu zetu waislamu wengine wote.

Ikiwa unaweza kutafuta nyumbani yako pekee basi fanya hivo. Ikiwa huwezi basi chagua chumba hapo nyumbani, jiweke ndani na jiepushe na mambo ya haramu. Hupati chochote katika dhambi zao. Midhali umekosa sehemu nyingine na huna pesa za kukodi sehemu, jiweke katika chumba maalum hapo nyumbani na waombee kwa Allaah awaongoze.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1326
  • Imechapishwa: 06/11/2019