Kujuzisha kuswali makaburini kwa kutumia hoja ´Aaishah kuswali nyumbani kwake

Swali: Vipi kumraddi mwenye kusema kuwa kuswali kwenye makaburi inajuzu kwa kutumia dalili ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kuswali nyumbani kwake?

Jibu: Nyumba yake haikuwa makaburini. Hii ni nyumba ya ´Aaishah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alizikwa ndani yake ili kumhifadhi na upetukaji mipaka. Nyumba yake sio makaburini. Huku ni kuchanganya mambo. Hakuwa anaenda kwenye kaburi hilo na kuswali pembezoni mwa kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Alikuwa anaswali kando kwenye nyumba yake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (01) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-1-30.mp3
  • Imechapishwa: 11/08/2020