Swali: Je, inajuzu kuingia sehemu ambazo nina dhana yenye nguvu kwamba kutakuwa maovu?

Jibu: Ikiwa utaweza kubadilisha maovu bila kupatikana maovu zaidi au kupelekea katika madhara, basi nenda ukakataze. Lakini ikiwa huwezi kuzuia kitu, basi haifai kwako kwenda au kukaa sehemu ambayo inasemekana kutakuwa maovu na wewe huwezi kubadilisha wala kuzuia.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (03) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/430/430.mp3
  • Imechapishwa: 26/03/2018