Linalomlazimu mzee ambaye aliacha kulipa madeni yake ya Ramadhaan kwa makusudi

Swali: Kuna mwanamke bibi kizee aliacha kulipa deni la Ramadhaan kwa muda mrefu pamoja na kwamba alikuwa anajua kuwa ni wajibu kwake kufanya hivo, lakini hata hivyo akaacha kulipa kwa uvivu. Hivi sasa ana maradhi ambayo hayamruhusu kuweza kufunga. Ni lipi linalomlazimu hivi sasa?

Jibu: Lililo wajibu kwake ni yeye kulisha kwa kila siku moja masikini. Kwa sababu ambalo lilikuwa ni wajibu kwake ni kulipa. Lakini ikiwa hawezi kwa kuwa na kizuizi ambacho hakitarajiwi kuondoka kutokana na utuuzima wake, ni wajibu kwake badala yake alishe kwa kila siku moja masikini.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (25)
  • Imechapishwa: 15/02/2019