Kufuta kanda na vitabu vilivyoandikwa “haki zote zimehifadhiwa”

Swali: Kanda ambazo zimeandikwa juu yake “Haki zote zimehifadhiwa” nikifuta maandishi haya inazingatiwa kuwa ni katika haki za watu ambazo watakuja kuziomba siku ya Qiyaamah?

Jibu: Ndugu! Kama wewe utakuwa na kanda na ukaandika kwamba haijuzu kwa mtu kunakili mpaka kwa idhini yako utaridhia aje mtu na kunakili bila ya idhini yako? Hutoridhia hili. Vipi basi wewe uwafanyie hivi wengine? Aliyeandika hivi haridhii yeyote afute isipokuwa kwa idhini yake au anunue kutoka kwako. Hii ni haki na jasho yako. Haijuzu kushambulia haki za watu na vitu vya watu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (07) http://alfawzan.af.org.sa/node/2122
  • Imechapishwa: 02/07/2020