Kufungua swawm kwa kula ili mtu aweze kufanya jimaa na kuepuka kafara

Swali: Tulikuwa katika kikao na baadhi ya ndugu na maongezi yetu yalikuwa yakizungumzia kuhusu swawm na baadhi ya mambo yenye kufunguza. Mmoja katika ndugu akasema kuwa amemsikia mtu akisema kwamba mtu akilazimika kufanya jimaa na mke wake mchana wa Ramadhaan ambapo akatanguliza kabla ya hapo kufungua kwa kula au kunywa basi anasalimika kutoa kafara kwa kufululiza kama ambaye amefanya jimaa mchana wa Ramadhaan. Je, haya yaliyosemwa na ndugu huyu ni sahihi?

Jibu: Maneno haya ni batili na sio sahihi. Ni wajibu kwa muislamu kutahadhari kufanya jimaa katika Ramadhaan midhali ni si mwenye kusafiri na mwenye afya njema. Vivyo hivyo linamuhusu mwanamke maadamu ni mwenye si mwenye kusafiri na mwenye afya njema.

Kuhusu msafiri hapana dhambi kumwingilia mke wake ambaye naye ni msafiri. Kadhalika mume mgonjwa akifanya na mke mgonjwa [hawana dhambi] ikiwa swawm ni yenye kuwatia uzito.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/309)
  • Imechapishwa: 01/06/2018