Kuchupa mpaka kwa Mtume (صلى الله عليه وسلم) kama inavofanywa katika maulidi

Watu wengi wamekwenda kinyume na makatazo yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Matokeo yake wakawa wanamuomba yeye, wanamtaka msaada, wanaapa kwa jina lake na wanamuomba mambo ambayo hayaombwi kutoka kwa yeyote isipokuwa Allaah pekee, kama inavofanywa katika maulidi, mashairi na Anaashiyd. Hawapambanui kati ya haki ya Allaah na haki ya Mtume. ´Allaamah Ibn-ul-Qayyim amesema katika an-Nuuniyyah:

Allaah ana haki isiyomwendea mwengine

mja pia ana haki – zinakuwa haki mbili

Hivyo usizifanye haki mbili hizo kuwa haki moja

pasi na kupambanua wala kutofautisha.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ´Aqiydat-ut-Tawhiyd, uk. 155
  • Imechapishwa: 17/11/2019