Swali: Wanawake wengi wanachukulia wepesi katika swalah zao ambapo inaonekana mikono yao au sehemu yake na vivyo hivyo miguu yake. Je, kipindi hicho swalah inasihi?
Jibu: Ni lazima kwa mwanamke muungwana ambaye ´ibaadah ni zenye kumuwajibikia kufunika mwili wake mzima ndani ya swalah usipokuwa uso na viganja vya mikono. Kwa sababu yeye wote ni ´awrah. Akiswali na ikaonekana sehemu ya ´awrah yake kama vile unyayo, mguu, kichwa au baadhi yake basi swalah yake haitosihi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah haikubali swalah ya mwenye hedhi isipokuwa kwa Khimaar.”
Ameipokea Ahmad na watunzi wa Sunan isipokuwa an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Makusudio ya mwenye hedhi ni yule ambaye amebaleghe.
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwanamke ni ´awrah.”
Abu Daawuud (Rahimahu Allaah) amepokea kupitia kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) aliyesimulia kwamba alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu mwanamke anayeswali kwenye shuka ya juu, Khimaar pasi na shuka ya chini akasema:
“Ikiwa shuka ya juu ni ndefu inafunika mguu mzima.”
Haafidhw Ibn Hajar (Rahimahu Allaah) amesema katika “Buluugh-ul-Maraam”:
“Maimamu wameona kuwa imesihi kutoka kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa).”
Akiwa mbele ya wanamme wa kando basi ni lazima kwake pia kufunika uso na viganja vya mikono.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/409)
- Imechapishwa: 02/10/2021
Swali: Wanawake wengi wanachukulia wepesi katika swalah zao ambapo inaonekana mikono yao au sehemu yake na vivyo hivyo miguu yake. Je, kipindi hicho swalah inasihi?
Jibu: Ni lazima kwa mwanamke muungwana ambaye ´ibaadah ni zenye kumuwajibikia kufunika mwili wake mzima ndani ya swalah usipokuwa uso na viganja vya mikono. Kwa sababu yeye wote ni ´awrah. Akiswali na ikaonekana sehemu ya ´awrah yake kama vile unyayo, mguu, kichwa au baadhi yake basi swalah yake haitosihi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah haikubali swalah ya mwenye hedhi isipokuwa kwa Khimaar.”
Ameipokea Ahmad na watunzi wa Sunan isipokuwa an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Makusudio ya mwenye hedhi ni yule ambaye amebaleghe.
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwanamke ni ´awrah.”
Abu Daawuud (Rahimahu Allaah) amepokea kupitia kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) aliyesimulia kwamba alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu mwanamke anayeswali kwenye shuka ya juu, Khimaar pasi na shuka ya chini akasema:
“Ikiwa shuka ya juu ni ndefu inafunika mguu mzima.”
Haafidhw Ibn Hajar (Rahimahu Allaah) amesema katika “Buluugh-ul-Maraam”:
“Maimamu wameona kuwa imesihi kutoka kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa).”
Akiwa mbele ya wanamme wa kando basi ni lazima kwake pia kufunika uso na viganja vya mikono.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/409)
Imechapishwa: 02/10/2021
https://firqatunnajia.com/kuchukulia-wepesi-wanawake-kufunika-mikono-na-miguu-katika-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)