Kuchelewesha swalah kwa wakati wake ni sawa na kutokuswali kabisa?

Swali 07: Kuchelewesha swalah kwa wakati wake hukumu yake ni sawa na kuiacha?

Jibu: Hapana. Ni jambo linahitajia upambanuzi. Si mamoja ikiwa ni kwa kusahau au kwa kupitikiwa na usingizi. Ama mtu akikusudia basi hukumu yake ni sawa na kuiacha kwa mujibu wa maoni sahihi. Basi katika hali hiyo mtu anakufuru endapo atakusudia kuichelewesha mpaka ukatoka wakati wake na wakati huohuo swalah hiyo ikawa haiwezi kukusanywa na ilio kabla na baada yake. Ama ikiwa swalah hiyo inaweza kukusanywa, basi hapa kuna utata. Wanachuoni wengi wanaona kuwa hukumu yake si sawa na kuiacha. Lakini hata hivyo anapata dhambi.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 32
  • Imechapishwa: 05/08/2018