Swali: Ni ipi hukumu ya kuashiria mkono ndani ya swalah wakati mtu anapotoa salamu na kumaliza swalah ambapo anageuza mikono na kusema:
السلام عليكم ورحمة الله وبركاته
“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kulia:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kushoto?
Jibu: Sunnah katika Tasliym mswaliji anatakiwa kusema:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kuliani mwake.
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kushotoni mwake. Asiashirie kwa mikono yake. Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa Jaabir bin Samurah ambaye amesema: “Niliswali pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na tulikuwa tunapotoa salamu tunaashiria kwa mikono yetu:
السلام عليكم السلام عليكم
“Amani ya Allaah iwe juu yenu. Amani ya Allaah iwe juu yenu.”
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akatutazama na akasema:
“Ni kwa nini mnaashiria kwa mikono yetu kana kwamba ni mikia ya farasi ilio na wasiwasi? Anapoleta Tasliym mmoja wenu basi ageukie upande wa mwenzake na wala asiashirie kwa mkono wake.”
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Bakr Abu Zayd
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (05/409) nr. (15441)
- Imechapishwa: 13/05/2022
Swali: Ni ipi hukumu ya kuashiria mkono ndani ya swalah wakati mtu anapotoa salamu na kumaliza swalah ambapo anageuza mikono na kusema:
السلام عليكم ورحمة الله وبركاته
“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kulia:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kushoto?
Jibu: Sunnah katika Tasliym mswaliji anatakiwa kusema:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kuliani mwake.
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
upande wa kushotoni mwake. Asiashirie kwa mikono yake. Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa Jaabir bin Samurah ambaye amesema: “Niliswali pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na tulikuwa tunapotoa salamu tunaashiria kwa mikono yetu:
السلام عليكم السلام عليكم
“Amani ya Allaah iwe juu yenu. Amani ya Allaah iwe juu yenu.”
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akatutazama na akasema:
“Ni kwa nini mnaashiria kwa mikono yetu kana kwamba ni mikia ya farasi ilio na wasiwasi? Anapoleta Tasliym mmoja wenu basi ageukie upande wa mwenzake na wala asiashirie kwa mkono wake.”
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalus-Shaykh
Bakr Abu Zayd
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (05/409) nr. (15441)
Imechapishwa: 13/05/2022
https://firqatunnajia.com/kuashiria-kwa-mikono-wakati-wa-tasliym/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)