Kuanza mihadhara na sherehe mbalimbali za kidini kwa kusoma Qur-aan

Swali: Ni yepi maoni yako kufungua mihadhara kwa kusoma Qur-aan tukufu? Je, hii ilikuwa ni miongoni mwa desturi za Salaf?

Jibu: Sijui kitu cha wazi juu ya hili. Isipokuwa ni kwamba ilikuwa ni miongoni mwa ada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapokusanyika na Maswahabah zake basi anasoma Qur-aan au anasomewa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kitendo ulichouliza ni katika sampuli hii. Hatujui kizuizi juu ya hilo. Ndani yake ipo kheri nyingi. Ni uzinduzi juu ya yale yanayonufaisha kutoka katika Qur-aan. Kitu bora cha kuyafungulia maneno ni Kitabu cha Allaah (´Azza wa Jall).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaad-ud-Duruus https://binbaz.org.sa/fatwas/4431/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%A8%D8%AF%D8%A1-%D8%A7%D9%84%D8%AC%D9%84%D8%B3%D8%A7%D8%AA-%D9%88%D8%A7%D9%84%D9%85%D8%AD%D8%A7%D8%B6%D8%B1%D8%A7%D8%AA-%D8%A8%D8%AA%D9%84%D8%A7%D9%88%D8%A9-%D8%A7%D9%8A%D8%A7%D8%AA
  • Imechapishwa: 20/09/2020