Swali: Ni ipi hukumu masomoni kusoma na kugusa Qur-aan wakati mwanamke yuko na hedhi?
Jibu: Haijuzu kwake kugusa Qur-aan moja kwa moja. Wanazuoni wametofautiana juu ya kusoma Qur-aan kwa hifdhi, lakini inafaa akihitajia kufanya hivo kama vile mtihani. Lakini hata hivyo asiguse Qur-aan moja kwa moja – ni lazima iwe nyuma ya kizuizi.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (28)
- Imechapishwa: 05/02/2022