Swali: Tunaomba kuwapa nasaha mwenzetu mmoja aliye na sisi ambaye anawakufurisha wanachuoni wa Sunnah mmoja wao akiwa ni Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz na Ibn ´Uthaymiyn (Rahimahumu Allaah) na kusema [sauti haiko wazi].

Jibu: Hili tumelijibu usiku wa jana na kusema kuwa watu kama hawa wapuuzwe. Dhambi hii inamrudilia yeye mwenyewe. Haliwadhuru wale aliyowatukana. Sisi tunawajua wanachuoni wetu na hatuna shaka juu yao. Maneno haya hayawaathiri. Kulisemwa juu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yalio makubwa kuliko hayo. Kadhalika kulisemwa juu ya maimamu wa Salaf yalio makubwa kuliko hayo. Hili lisiwashangaze. Msishangazwe kukawa vipingamizi na mashambulizi mbali mbali kwenye haki na watu wa haki wakatukanywa na kuhujumiwa. Hili halishangazi. Msijali hili.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (03) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_03.mp3
  • Imechapishwa: 02/07/2018