Khatari na madhara juu ya Ummah kwa wenye kujifanya kuwa ni wanachuoni

Swali: Kuna Khutbah moja ambapo Khatwiyb alituswalisha na akatutolea Khutbah moja kutokana na ujinga wake au kwa kusahau. Ni ipi hukumu ya swalah yetu?

Jibu: Tunamuomba Allaah afya. Si kwamba ni ujinga au amesahau. Wanakusudia kufanya hivi. Hawa wanajifanya kama ni wanachuoni. Ni watu wamejitokeza kwa watu na lengo lao ni kutaka kwenda kinyume na yale waliyomo wengine na moja katika mambo hayo ni kwamba wanatoa Khutbah moja. Ijumaa haisihi isipokuwa kwa Khutbah mbili kama ambavyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyokuwa akifanya, makhaliyfah wake na waislamu wengine wote. Hili ni kwa Ijmaa´. Haijuzu upinzani kama huu.

Watu hawa wanaojifanya ni wanachuoni ni khatari kwa Ummah. Watu hawa kunachelea juu yao wakaja kuupotosha Ummah. Ni wajibu wakachukuliwa hatua.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (58) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-01-14.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020