Swali: Ninapoingia msikitini na nikamkuta imamu anasoma al-Faatihah nisome du´aa ya kufungulia swalah au hapana?
Jibu: Unapojiunga na imamu na ukamkuta imamu anasoma al-Faatihah, basi kati ya al-Faatihah na kusomwa kwa Suurah nyingine au kinyamazo – kama inavokuwa mara nyingi – tunakwambia kuwa unatakiwa sasa kunyamaza kwa sababu ya kisomo cha imamu. Atapomaliza kusoma al-Faatihah soma du´aa ya kufungulia swalah kisha ndio usome al-Faatihah hata kama imamu atakuwa anasoma.
Lakini ukichelea kuwa hatonyamaza kati ya al-Faatihah na kusoma Suurah nyingine au ukachelea atasoma Suurah fupi ambayo haitokuwezesha kusoma al-Faatihah, basi pale tu utapojiunga naye unatakiwa kusema “Allaahu Akbar” na useme:
أعوذ بالله من الشيطان الرجيم
“Najilinda kwa Allaah kutokamana na shaytwaan aliyefukuzwa.”
kisha ndio usome al-Faatihah. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikataza mswaliji kusoma na huku imamu yuko anasoma isipokuwa tu al-Faatihah.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (40) http://binothaimeen.net/content/913
- Imechapishwa: 22/09/2018
Swali: Ninapoingia msikitini na nikamkuta imamu anasoma al-Faatihah nisome du´aa ya kufungulia swalah au hapana?
Jibu: Unapojiunga na imamu na ukamkuta imamu anasoma al-Faatihah, basi kati ya al-Faatihah na kusomwa kwa Suurah nyingine au kinyamazo – kama inavokuwa mara nyingi – tunakwambia kuwa unatakiwa sasa kunyamaza kwa sababu ya kisomo cha imamu. Atapomaliza kusoma al-Faatihah soma du´aa ya kufungulia swalah kisha ndio usome al-Faatihah hata kama imamu atakuwa anasoma.
Lakini ukichelea kuwa hatonyamaza kati ya al-Faatihah na kusoma Suurah nyingine au ukachelea atasoma Suurah fupi ambayo haitokuwezesha kusoma al-Faatihah, basi pale tu utapojiunga naye unatakiwa kusema “Allaahu Akbar” na useme:
أعوذ بالله من الشيطان الرجيم
“Najilinda kwa Allaah kutokamana na shaytwaan aliyefukuzwa.”
kisha ndio usome al-Faatihah. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikataza mswaliji kusoma na huku imamu yuko anasoma isipokuwa tu al-Faatihah.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (40) http://binothaimeen.net/content/913
Imechapishwa: 22/09/2018
https://firqatunnajia.com/katika-hali-hii-kunasomwa-duaa-ya-kufungulia-swalah-au-al-faatihah-moja-kwa-moja/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)