Kafiri amesilimu na anamtaka mke wake baada ya kuwa kishaolewa

Swali: Mwanamke muolewaji akisilimu na akaolewa na muislamu mmoja. Kisha baada ya muda akasilimu mume wake wa kwanza…

Jibu: Hana lolote tena kuhusiana na yeye. Mwanamke huyu akishaolewa mambo yamekwisha na hana lolote tena kuhusiana na yeye. Lakini muislamu asimuoe mpaka atoke ndani ya eda. Kwa kuwa lau mume wake atasilimu na yeye bado yumo ndani ya eda, anarudi kwake. Akitoka ndani ya eda na akawa hajasilimu, anatengana naye. Katika hali hiyo inajuzu kwa muislamu kumuoa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (53) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1432-06-12.mp3
  • Imechapishwa: 16/11/2014