Kafara kwa aliyechelewesha kulipa deni

Swali: Muulizaji kutoka Uswidi. Kuna mtu ambaye hakufunga siku ishirini katika Ramadhaan iliyopita kwa sababu ya maradhi. Lakini alikuwa anaweza baada ya Ramadhaan na hakufunga mpaka ikaingia Ramadhana nyingine. Juu yake ana nini?

Jibu:  Atafunga Ramadhaan kisha siku hizi zilizobaki baada ya Ramadhaan atazilipa pamoja na kulisha.

  • Mhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://alwasabi.al3ilm.com/alfatawaa
  • Imechapishwa: 10/05/2020