Swali: Katika mji wetu kumekithiri kuyaabudu makaburi. Baadhi ya walinganizi hawajali kuyakataza mambo kama haya. Unatunasihi nini sisi na wao juu ya suala kama hili?
Jibu: Kuwabainishia, kuwafunza na kuwaelekeza. Allaah atamwongoza amtakaye. Nanyi mtalipwa ujira. Ama kuwanyamazia na kuwaacha, Allaah atakuulizeni siku ya Qiyaamah. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
وَمَا كَانَ الْمُؤْمِنُونَ لِيَنفِرُوا كَافَّةً ۚ فَلَوْلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرْقَةٍ مِّنْهُمْ طَائِفَةٌ لِّيَتَفَقَّهُوا فِي الدِّينِ وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ
“Haiwapasi waumini watoke wote pamoja kwenda [katika Jihaad]. Basi ni kwanini lisitoke katika kila kundi miongoni mwao kundi moja wajifunze dini na ili waonye watu wao watakaporudi kwao ili wapate kutahadhari.”[1]
Inawahusu wanafunzi. Hili ndilo jukumu lenu; kueneza dini, kueneza ulinganizi kwa Allaah (´Azza wa Jall) na kuwafunza watu.
[1] 09:122
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (61) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20majid-%2029%20-0%206-1438.mp3
- Imechapishwa: 06/08/2017
Swali: Katika mji wetu kumekithiri kuyaabudu makaburi. Baadhi ya walinganizi hawajali kuyakataza mambo kama haya. Unatunasihi nini sisi na wao juu ya suala kama hili?
Jibu: Kuwabainishia, kuwafunza na kuwaelekeza. Allaah atamwongoza amtakaye. Nanyi mtalipwa ujira. Ama kuwanyamazia na kuwaacha, Allaah atakuulizeni siku ya Qiyaamah. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
وَمَا كَانَ الْمُؤْمِنُونَ لِيَنفِرُوا كَافَّةً ۚ فَلَوْلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرْقَةٍ مِّنْهُمْ طَائِفَةٌ لِّيَتَفَقَّهُوا فِي الدِّينِ وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ
“Haiwapasi waumini watoke wote pamoja kwenda [katika Jihaad]. Basi ni kwanini lisitoke katika kila kundi miongoni mwao kundi moja wajifunze dini na ili waonye watu wao watakaporudi kwao ili wapate kutahadhari.”[1]
Inawahusu wanafunzi. Hili ndilo jukumu lenu; kueneza dini, kueneza ulinganizi kwa Allaah (´Azza wa Jall) na kuwafunza watu.
[1] 09:122
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (61) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20majid-%2029%20-0%206-1438.mp3
Imechapishwa: 06/08/2017
https://firqatunnajia.com/jukumu-la-wanafunzi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)