Jukumu la wanachuoni na walinganizi dhidi ya Raafidhwah

Swali: Raafidhwah khatari yao ni kubwa na imefika. Ni yepi majukumu ya wanachuoni na wanafunzi juu ya kuzindua khatari hii?

Jibu: Ni wajibu kwa wanachuoni kubainisha I´tiqaad batili zinazopingana na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah kukiwemo vilevile ´Aqiydah ya Raafidhwah, Mu´tazilah, Jahmiyyah na Khawaarij. Zote hizi ni I´tiqaad potofu na mbovu. Lililo la wajibu ni kuzindua na kubainisha haki na kusambaratisha batili ili muumini awe juu ya ujuzi.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (02) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/429/429.mp3
  • Imechapishwa: 01/03/2018