Jione daima uko duni kuliko wengine wote

Swali: Kupenda sifa na matapo kwa watu ni jambo lenye kusemwa vibaya kwa hali yoyote?

Jibu: Ndio, ni jambo lenye kusemwa vibaya kwa hali yoyote. Mtu asipende kusifiwa na kutapwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kumsifu mtu mbele yake:

“Mkiwaona wenye kusifu watupieni kwenye nyuso zao mchanga.”

Kwa sababu jambo hili linapelekea kujikweza na kujiona. Mtu anatakiwa kujiona kuwa ni mwenye mapungufu na ajione kuwa yuko duni kuliko wengine. Asijinyanyue.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (72) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-10-14.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020