Swali: Mwanamke huyu anasema kwamba amedangana sana. Ametekeleza faradhi ya hajj – na himdi zote anastahiki Allaah – lakini kinachonifanya kudangana na kuwa na wasiwasi juu ya upungufu wa hajj yangu ni kwamba mimi sikugharamikia zile thamani zake. Aliyegharamikia hayo ni mmoja katika wahisani kwa sababu mshahara wa mume wangu ulikuwa mdogo. Mimi wakati huo nilikuwa namiliki dhahabu kidogo. Nachelea hajj yangu isije kuwa yenye mapungufu kwa sababu sikuuza dhahabu hii ili nigharamikie gharama hizo.
Jibu: Hajj sio pungufu – Allaah akitaka. Nataraji kwa Allaah kwamba ni yenye kukubaliwa. Wala sio lazima kuuza dhahabu yake ili aweze kuhiji. Kwa sababu dhahabu ni miongoni mwa mahitajio ya kimaumbile ambayo ni lazima mwanamke awe nayo. Kwa hiyo sio lazima aiuze ili aweze kuhiji. Hivyo namwambia mwanamke huyu: tulia! Hajj yako ni sahihi na umetekeleza dhimma yako. Umeshatekeleza faradhi.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (42) http://binothaimeen.net/content/981
- Imechapishwa: 28/12/2018
Swali: Mwanamke huyu anasema kwamba amedangana sana. Ametekeleza faradhi ya hajj – na himdi zote anastahiki Allaah – lakini kinachonifanya kudangana na kuwa na wasiwasi juu ya upungufu wa hajj yangu ni kwamba mimi sikugharamikia zile thamani zake. Aliyegharamikia hayo ni mmoja katika wahisani kwa sababu mshahara wa mume wangu ulikuwa mdogo. Mimi wakati huo nilikuwa namiliki dhahabu kidogo. Nachelea hajj yangu isije kuwa yenye mapungufu kwa sababu sikuuza dhahabu hii ili nigharamikie gharama hizo.
Jibu: Hajj sio pungufu – Allaah akitaka. Nataraji kwa Allaah kwamba ni yenye kukubaliwa. Wala sio lazima kuuza dhahabu yake ili aweze kuhiji. Kwa sababu dhahabu ni miongoni mwa mahitajio ya kimaumbile ambayo ni lazima mwanamke awe nayo. Kwa hiyo sio lazima aiuze ili aweze kuhiji. Hivyo namwambia mwanamke huyu: tulia! Hajj yako ni sahihi na umetekeleza dhimma yako. Umeshatekeleza faradhi.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (42) http://binothaimeen.net/content/981
Imechapishwa: 28/12/2018
https://firqatunnajia.com/je-thawabu-za-hajj-zinapungua-mtu-akisafiri-kwa-gharamu-za-mtu-mwingine/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)