Enyi watu wenye chuki kwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah! Miongoni mwa sifa kuu za Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni inswafu na uadilifu. Wanawaita Murji-ah wa kikweli “Murji-ah” kwa kuwa wanayaondosha matendo katika imani. Kwa mujibu wa baadhi yao imani ni kule kuwa na utambuzi peke yake na wengine wanasema kuwa imani ni maneno pasi na matendo yoyote. Murji-ah al-Fuqahaa´ wanasema kuwa imani ni kusadikisha kwa moyo na kutamka kwa ulimi. Wote ni wenye kukubaliana juu ya kuyaondosha matendo katika imani, ya kwamba haizidi na wala haipungui, kwamba mtenda dhambi mkubwa ana imani sawa na Jibriyl na Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kwamba imani haitofautiani kati ya watu. Je, mmepata ´Aqiydah hii ya kipotevu kwa Ahl-us-Sunnah ambao mnawapiga vita na kuwatuhumu Irjaa´ na Irjaa´ iliyopindukia?

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kashf Akaadhiyb wa Tahriyfaat wa Khiyaanaat Fawziy al-Bahrayniy, uk. 33-34
  • Imechapishwa: 09/10/2016