´Iysaa ndiye mbora wa Ummah huu

Swali:  Je, mtu anaweza kusema kuwa ´Iysaa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Swahabah?

Jibu: ´Iysaa ni Nabii na ni mbora kuliko Swahabah. Atateremka katika zama za mwisho na ni moja katika alama kubwa za Qiyaamah. Atahukumu kwa Shari´ah ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ni mmoja katika watu wa Ummah huu wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ndiye mtu mbora wa Ummah huu baada ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha anafuata Abu Bakr.

  • Mhusika: Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ataawaa Mutanawwi´ah (03) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/430/430.mp3
  • Imechapishwa: 22/06/2018